< Zaburi 45 >

1 Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
For the end, for alternate [strains] by the sons of Core; for instruction, a Song concerning the beloved. My heart has uttered a good matter: I declare my works to the king: my tongue is the pen of a quick writer.
2 Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
You are more beautiful than the sons of men: grace has been shed forth on your lips: therefore God has blessed you for ever.
3 Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
Gird your sword upon your thigh, O Mighty One, in your comeliness, and in your beauty;
4 Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
and bend [your bow], and prosper, and reign, because of truth and meekness and righteousness; and your right hand shall guide you wonderfully.
5 Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
Your weapons are sharpened, Mighty One, (the nations shall fall under you) [they are] in the heart of the king's enemies.
6 Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
Your throne, O God, is for ever and ever: the sceptre of your kingdom is a sceptre of righteousness.
7 Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
You have loved righteousness, and hated iniquity: therefore God, your God, has anointed you with the oil of gladness beyond your fellows.
8 Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
Myrrh, and stacte, and cassia [are exhaled] from your garments, [and] out of the ivory palaces,
9 Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
with which kings' daughters have gladdened you for your honour: the queen stood by on your right hand, clothed in vesture wrought with gold, [and] arrayed in various colours.
10 Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
Hear, O daughter, and see, and incline your ear; forget also your people, and your father's house.
11 Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
Because the king has desired your beauty; for he is your Lord.
12 Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
And the daughter of Tyre shall adore him with gifts; the rich of the people of the land shall supplicate your favour.
13 Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
All her glory [is that] of the daughter of the king of Esebon, robed [as she is] in golden fringed garments,
14 Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
in embroidered [clothing]: virgins shall be brought to the king after her: her fellows shall be brought to you.
15 Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
They shall be brought with gladness and exultation: they shall be led into the king's temple.
16 Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
Instead of your fathers children are born to you: you shall make them princes over all the earth.
17 Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.
They shall make mention of your name from generation to generation: therefore shall the nations give thanks to you for ever, even for ever and ever.

< Zaburi 45 >