< Zaburi 45 >
1 Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
For the choirmaster. To the tune of “The Lilies.” A Maskil of the sons of Korah. A love song. My heart is stirred by a noble theme as I recite my verses to the king; my tongue is the pen of a skillful writer.
2 Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
You are the most handsome of men; grace has anointed your lips, since God has blessed you forever.
3 Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
Strap your sword at your side, O mighty warrior; appear in your majesty and splendor.
4 Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
In your splendor ride forth in victory on behalf of truth and humility and justice; may your right hand show your awesome deeds.
5 Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
Your arrows pierce the hearts of the king’s foes; the nations fall beneath your feet.
6 Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
Your throne, O God, endures forever and ever, and justice is the scepter of Your kingdom.
7 Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
You have loved righteousness and hated wickedness; therefore God, your God, has anointed you above your companions with the oil of joy.
8 Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
All your garments are fragrant with myrrh and aloes and cassia; from palaces of ivory the harps make you glad.
9 Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
The daughters of kings are among your honored women; the queen stands at your right hand, adorned with the gold of Ophir.
10 Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
Listen, O daughter! Consider and incline your ear: Forget your people and your father’s house,
11 Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
and the king will desire your beauty; bow to him, for he is your lord.
12 Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
The Daughter of Tyre will come with a gift; men of wealth will seek your favor.
13 Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
All glorious is the princess in her chamber; her gown is embroidered with gold.
14 Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
In colorful garments she is led to the king; her virgin companions are brought before you.
15 Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
They are led in with joy and gladness; they enter the palace of the king.
16 Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
Your sons will succeed your fathers; you will make them princes throughout the land.
17 Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.
I will commemorate your name through all generations; therefore the nations will praise you forever and ever.