< Zaburi 44 >
1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
Al Músico principal: de los hijos de Coré: Masquil. OH Dios, con nuestros oídos hemos oído, nuestros padres nos han contado, la obra que hiciste en sus días, en los tiempos antiguos.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
Tú con tu mano echaste las gentes, y los plantaste á ellos; afligiste los pueblos, y los arrojaste.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
Porque no se apoderaron de la tierra por su espada, ni su brazo los libró; sino tu diestra, y tu brazo, y la luz de tu rostro, porque te complaciste en ellos.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
Tú, oh Dios, eres mi rey: manda saludes á Jacob.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
Por medio de ti sacudiremos á nuestros enemigos: en tu nombre atropellaremos á nuestros adversarios.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
Porque no confiaré en mi arco, ni mi espada me salvará.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
Pues tú nos has guardado de nuestros enemigos, y has avergonzado á los que nos aborrecían.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
En Dios nos gloriaremos todo tiempo, y para siempre loaremos tu nombre. (Selah)
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
Empero [nos] has desechado, y nos has hecho avergonzar; y no sales en nuestros ejércitos.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
Nos hiciste retroceder del enemigo, y saqueáron[nos] para sí los que nos aborrecían.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
Pusístenos como á ovejas para comida, y esparcístenos entre las gentes.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
Has vendido tu pueblo de balde, y no pujaste en sus precios.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
Pusístenos por vergüenza á nuestros vecinos, por escarnio y por burla á los que nos rodean.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
Pusístenos por proverbio entre las gentes, por movimiento de cabeza en los pueblos.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
Cada día mi vergüenza está delante de mí, y cúbreme la confusión de mi rostro,
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
Por la voz del que [me] vitupera y deshonra, por razón del enemigo y del que se venga.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
Todo esto nos ha venido, y no nos hemos olvidado de ti; y no hemos faltado á tu pacto.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
No se ha vuelto atrás nuestro corazón, ni tampoco se han apartado nuestros pasos de tus caminos.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
Cuando nos quebrantaste en el lugar de los dragones, y nos cubriste con sombra de muerte,
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
Si nos hubiésemos olvidado del nombre de nuestro Dios, ó alzado nuestras manos á dios ajeno,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
¿No demandaría Dios esto? porque él conoce los secretos del corazón.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
Empero por tu causa nos matan cada día; somos tenidos como ovejas para el matadero.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Despierta; ¿por qué duermes, Señor? Despierta, no te alejes para siempre.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
¿Por qué escondes tu rostro, y te olvidas de nuestra aflicción, y de la opresión nuestra?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
Porque nuestra alma está agobiada hasta el polvo: nuestro vientre está pegado con la tierra.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Levántate para ayudarnos, y redímenos por tu misericordia.