< Zaburi 44 >
1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
God, we ourselves have heard what our parents and grandparents told us. They told us about the miracles that you performed long ago.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
[They told us] how you expelled the ungodly people and enabled us to live in their land. [They told us] that you punished those ungodly people and enabled your own people to prosper [IDM].
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
It was not by using their own swords that they conquered the people that lived in that land, and it was not by their own power that they were victorious; it was only by your power [MTY, DOU] [that they did those things]; and they were sure that you were with them, and that showed that you were pleased with them.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
You are my King and my God; it is you who enable us, your people [MTY], to defeat our enemies.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
It is by your power that we knock our enemies down and tramp on them.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
I do not trust that I will be saved by using my bow [and arrows] and my sword.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
No, it is you who have rescued us from our enemies, it is you who have caused those who hate us to become ashamed [because they were defeated].
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
We have continually boasted about what God [has done for us], and we will thank him [MTY] forever.
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
But [now] you have rejected us and caused us to be disgraced; when our armies march out [to fight a battle], you no [longer] go with them.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
You have caused us to run away from our enemies, with the result that they captured the things that belonged to us.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
You have allowed us to become like [MET] sheep that were ready to be slaughtered; you scattered us [far away] among [other].
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
[It is as though] [MET] you sold us, your people, [to our enemies] for a very small price, and you did not gain much profit from selling us!
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
People who live in nations near us make fun of us; they laugh at us and deride/belittle us.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
They make jokes using the name of [our country], they shake their heads [to indicate that they despise us].
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
All day I feel disgraced; from seeing my face, people know that I am ashamed.
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
I hear what those who sneer at me and revile me say; I am ashamed in front of my enemies and those who want to harm me.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
All these things have happened to us [even] though we have not forgotten you, and we are not the ones who disobeyed the agreement you made with [our ancestors].
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
We have not stopped being loyal to you, and we have not stopped doing what you want us to do [IDM].
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
But [it is as though] you have allowed us to be helpless among wild animals, and abandoned us in a deep dark [ravine].
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
If we had forgotten to worship [MTY] our God, or if we had spread out our hands to [worship] a foreign god,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
you certainly would have known that, because you know [even] what we secretly think.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
But it is because we belong to you, [that our enemies] are constantly killing us. They act toward us as though we were only sheep to be slaughtered.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
[So], Yahweh, arise! Why are you asleep [RHQ]? Get up! Do not reject us forever!
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Why are you not looking at us? Why are you forgetting that we are suffering and being oppressed [by our enemies]?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
We are pushed down to the ground and we cannot get up.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Arise, and come and help us! Rescue us because you faithfully love us!