< Zaburi 44 >
1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
“To the chief musician, for the sons of Korach, a Maskil.” O God, with our ears have we heard, our fathers have told us, deeds which thou hadst done in their days, in times of old.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
Thou, with thy hand, didst indeed drive out nations, and plant them; thou didst ill-treat people, and cause them to spread out.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
For not by their sword did they obtain possession of the land, and their own arm brought them no victory; but thy right hand, and thy arm, and the light of thy countenance, because thou hadst given them thy favor.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
Thou art my King, O God: ordain salvation for Jacob.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
Through thee will we butt down our assailants: through thy name will we tread under foot our opponents.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
For not in my bow will I trust, and my sword shall not help me.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
But thou helpest us against our assailants, and those that hate us thou puttest to shame.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
Of God we boast all the day, and to thy name will we give thanks for ever. (Selah)
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
But [now] thou hast cast off, and put us to the blush, and goest not forth with our armies.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
Thou causest us to turn back from before our assailant: and they who hate us take spoil for themselves.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
Thou givest us up like sheep for food, and among the nations hast thou dispersed us.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
Thou sellest thy people for no value, and acquirest no gain by their price.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
Thou renderest us a reproach to our neighbors, a scorn and a derision to those that are round about us.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
Thou renderest us a by-word among the nations, a shaking of the head among the people.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
All the day is my disgrace before me, and the shame of my face covereth me;
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
Because of the voice of him that reproacheth and blasphemeth; by reason of the enemy and him that seeketh vengeance.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
All this is come over us, yet have we not forgotten thee; nor have we dealt falsely by thy covenant;
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Our heart is not moved backward, nor hath our step turned aside from thy path:
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
Even when thou didst crush us in the abode of monsters, and cover us with the shadow of death.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
If we had forgotten the name of our God, or spread forth our hands to a strange God:
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
Would not God search out this? for he knoweth the secrets of the heart.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
But for thy sake are we slain all the day; we are counted as flocks [destined] for slaughter.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Awake, wherefore wilt thou sleep, O Lord? arise, abandon us not for ever.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Wherefore wilt thou hide thy face, wilt thou forget our misery, and our oppression?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
For our soul is bowed down to the dust; our body cleaveth unto the earth.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Arise unto our help, and redeem us for the sake of thy kindness.