< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
For the choirmaster. A Maskil of the sons of Korah. We have heard with our ears, O God; our fathers have told us the work You did in their days, in the days of old.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
With Your hand You drove out the nations and planted our fathers there; You crushed the peoples and cast them out.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
For it was not by their sword that they took the land; their arm did not bring them victory. It was by Your right hand, Your arm, and the light of Your face, because You favored them.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
You are my King, O God, who ordains victories for Jacob.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
Through You we repel our foes; through Your name we trample our enemies.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
For I do not trust in my bow, nor does my sword save me.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
For You save us from our enemies; You put those who hate us to shame.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
In God we have boasted all day long, and Your name we will praise forever.
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
But You have rejected and humbled us; You no longer go forth with our armies.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
You have made us retreat from the foe, and those who hate us have plundered us.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
You have given us up as sheep to be devoured; You have scattered us among the nations.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
You sell Your people for nothing; no profit do You gain from their sale.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
You have made us a reproach to our neighbors, a mockery and derision to those around us.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
You have made us a byword among the nations, a laughingstock among the peoples.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
All day long my disgrace is before me, and shame has covered my face,
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
at the voice of the scorner and reviler, because of the enemy, bent on revenge.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
All this has come upon us, though we have not forgotten You or betrayed Your covenant.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Our hearts have not turned back; our steps have not strayed from Your path.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
But You have crushed us in the lair of jackals; You have covered us with deepest darkness.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
If we had forgotten the name of our God or spread out our hands to a foreign god,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
would not God have discovered, since He knows the secrets of the heart?
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
Yet for Your sake we face death all day long; we are considered as sheep to be slaughtered.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Wake up, O Lord! Why are You sleeping? Arise! Do not reject us forever.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Why do You hide Your face and forget our affliction and oppression?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
For our soul has sunk to the dust; our bodies cling to the earth.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Rise up; be our help! Redeem us on account of Your loving devotion.

< Zaburi 44 >