< Zaburi 42 >
1 Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
Pour le chef musicien. Une contemplation par les fils de Korah. Comme le cerf s'impatiente devant les ruisseaux, ainsi mon âme se languit de toi, Dieu.
2 Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
Mon âme a soif de Dieu, du Dieu vivant. Quand vais-je venir me présenter devant Dieu?
3 Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Mes larmes ont été ma nourriture jour et nuit, alors qu'ils me demandent sans cesse: « Où est ton Dieu? »
4 Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
Je me souviens de ces choses, et je répands mon âme en moi, comment j'avais l'habitude d'aller avec la foule, et de les conduire à la maison de Dieu, avec la voix de la joie et de la louange, une multitude célébrant un jour saint.
5 Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
Pourquoi es-tu désespéré, mon âme? Pourquoi es-tu troublé en moi? L'espoir en Dieu! Car je le louerai encore pour l'aide salvatrice de sa présence.
6 Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
Mon Dieu, mon âme est désespérée au-dedans de moi. C'est pourquoi je me souviens de toi depuis le pays du Jourdain, les hauteurs de l'Hermon, de la colline Mizar.
7 Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
Deep appelle à Deep au bruit de vos chutes d'eau. Toutes tes vagues et tous tes flots m'ont balayé.
8 Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
L'Éternel commandera sa bonté pendant le jour. Dans la nuit, sa chanson sera avec moi: une prière au Dieu de ma vie.
9 Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
Je demanderai à Dieu, mon rocher: « Pourquoi m'as-tu oublié? Pourquoi suis-je en deuil à cause de l'oppression de l'ennemi? »
10 Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
Comme une épée dans mes os, mes adversaires m'outragent, alors qu'ils me demandent sans cesse: « Où est ton Dieu? »
11 Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.
Pourquoies-tu désespéré, mon âme? Pourquoi es-tu troublé en moi? Espère en Dieu! Car je le louerai encore, l'aide salvatrice de mon visage, et mon Dieu.