< Zaburi 42 >

1 Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
“BOOK II. For the leader of the music. A song of the sons of Korah.” As the hart panteth for the water-brooks, So panteth my soul for thee, O God!
2 Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
My soul thirsteth for God, the living God: When shall I come, and appear before God?
3 Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
My tears have been my food day and night, While they say to me continually, “Where is thy God?”
4 Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
When I think of it, I pour out my soul in grief; How I once walked with the multitude, Walked slowly with them to the house of God, Amid sounds of joy and praise with the festive multitude!
5 Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
Why art thou cast down, O my soul? And why art thou disquieted within me? Hope thou in God; for I shall yet praise him, Him, my deliverer and my God!
6 Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
My soul is cast down within me, While I remember thee from the land of Jordan and Hermon, From the mountain Mizar.
7 Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
Deep calleth for deep at the noise of thy waterfalls; All thy waves and billows have gone over me!
8 Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
Once the LORD commanded his kindness by day, And by night his praise was with me, -Thanksgiving to the God of my life.
9 Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
Now I say to God, my rock, Why hast thou forgotten me? Why go I mourning on account of the oppression of the enemy?
10 Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
Like the crushing of my bones are the reproaches of the enemy, While they say to me continually, “Where is thy God?”
11 Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.
Why art thou cast down, O my soul? And why art thou disquieted within me? Hope thou in God; for I shall yet praise him, Him, my deliverer and my God!

< Zaburi 42 >