< Zaburi 42 >

1 Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
For the music director. A psalm (maskil) of the sons of Korah. As a deer longs for flowing streams, so I long for you, God.
2 Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
I am thirsty for God, the living God. When can I go and see God's face?
3 Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
My tears have been my only food, day and night, while people ask me all day long, “Where is your God?”
4 Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
I am crushed as I remember how I walked with the crowds, leading them in a procession to the house of God, with shouts of joy and songs of thanks among the worshipers at the festival.
5 Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
Why am I so discouraged? Why do I feel so sad? I will hope in God; I will praise him because he is the one who saves me—
6 Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
my God! Even though I am very discouraged, I still remember you: from the land of Jordan and Hermon, and from Mount Mizar.
7 Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
You thunder through the raging waters, through the noise of the waterfalls. Your crashing waves surge over me—I feel like I'm drowning.
8 Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
But every day the Lord shows me his trustworthy love; every night he gives me songs to sing—a prayer to the God of my life.
9 Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
I cry out, “My God, my rock, why have you forgotten me? Why must I go around weeping because of the attacks of my enemies?”
10 Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
The mocking of my attackers crushes my bones. They're always asking me, “Where is your God?”
11 Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.
Why am I so discouraged? Why do I feel so sad? I will hope in God; I will praise him because he is the one who saves me—my God!

< Zaburi 42 >