< Zaburi 41 >
1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
Pour le chef musicien. Un psaume de David. Béni soit celui qui considère les pauvres. Yahvé le délivrera au jour du malheur.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
L'Éternel le protégera et le fera vivre. Il sera béni sur la terre, et il ne le livrera pas à la volonté de ses ennemis.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
Yahvé le soutiendra sur son lit de malade, et le faire sortir de son lit de maladie.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
J'ai dit: « Yahvé, aie pitié de moi! Guéris-moi, car j'ai péché contre toi. »
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
Mes ennemis disent du mal de moi: « Quand mourra-t-il, et son nom périra-t-il? »
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
S'il vient me voir, il dit des mensonges. Son cœur rassemble l'iniquité à lui. Quand il va à l'étranger, il le raconte.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
Tous ceux qui me haïssent murmurent ensemble contre moi. Ils imaginent le pire pour moi.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
« Une mauvaise maladie », disent-ils, « l'a affligé ». Maintenant qu'il est couché, il ne se relèvera plus. »
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
Oui, mon ami familier, en qui j'avais confiance, qui ont mangé du pain avec moi, a levé son talon contre moi.
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
Mais toi, Yahvé, aie pitié de moi, et relève-moi, pour que je leur rende la pareille.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
Je sais par là que tu te plais en moi, car mon ennemi ne triomphe pas de moi.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
Quant à moi, tu me soutiens dans mon intégrité, et me mettre en ta présence pour toujours.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Bénisoit Yahvé, le Dieu d'Israël, de l'éternité et à l'éternité! Amen et amen.