< Zaburi 41 >

1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
To the Chief Musician. A Melody of David. How happy is he that is attentive to the poor, In the day of calamity, will Yahweh deliver him:
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
Yahweh, will preserve him and keep him alive, And he shall be pronounced happy in the land, Do not then give him up at the desire of his enemies!
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
Yahweh, will sustain him upon the bed of sickness, All his couch, hast thou transformed in his disease.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
I, said—O Yahweh, show me favour, heal thou my soul, for I have sinned against thee:
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
Mine enemies, speak ill of me, When will he die, and his name perish?
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
And, if he have come to see me, Falsehood, doth he speak, His own heart, gathereth iniquity to itself, he goeth forth, abroad he telleth it.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
Together—against me, do all who hate me whisper among themselves, Against me, devise they hurt for me.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
An infliction of the Abandoned One hath been fixed upon him, and, now that he hath lien down, he will not again rise.
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
Even the man whom I used to salute, in whom I put confidence, who used to eat my bread, —hath magnified his heel against me!
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
But, thou, O Yahweh, show me favour and raise me up, That I may repay them.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
Hereby, do I know that thou delightest in me, In that mine enemy shall not raise a shout over me.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
But, as for me, In my blamelessness, hast thou held me fast, And hast caused me to stand before thee unto times age-abiding.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed be Yahweh, the God of Israel, From the age that is past, even unto the age yet to come: Amen and Amen!

< Zaburi 41 >