< Zaburi 41 >
1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
For the leader; for Jeduthun. A psalm of David. Happy are those who consider the weak; in the day of misfortune the Lord will deliver them.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
He will keep them safe, happy, and long in the land, and not give them up to the rage of their foes.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
The Lord will sustain them on bed of languishing; tending their sickness, as long as they lie.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
For this cause I say, “Lord, show me your favor; heal me, because I have sinned against you.”
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
My enemies speak of me nothing but evil, “When will he die, and his name pass away?”
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
When one comes to see me, their words ring hollow; their heart keeps gathering mischief the while; and when they go out, they give it speech.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
In secret they whisper together against me, all those who hate me plot evil against me.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
“Some fatal disease has fastened upon him; and now that he lies, he will rise up no more.”
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
My most trusted friend, on whom I relied, who ate of my bread, has turned against me.
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
But do you, Lord, graciously raise me up, that I may pay them their due reward.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
By this will I know you delight in me: if my foes may not shout over me in triumph.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
For my innocence you uphold me, and set me forever before your face.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed be the Lord, the God of Israel, from everlasting to everlasting, Amen and Amen.