< Zaburi 41 >

1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
TO THE OVERSEER. A PSALM OF DAVID. O the blessedness of him Who is acting wisely to the poor, In a day of evil YHWH delivers him.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
YHWH preserves him and revives him, He is blessed in the land, And You do not give him into the will of his enemies.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
YHWH supports [him] on a bed of sickness, You have turned his bed in his weakness.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, “O YHWH, favor me, Heal my soul, for I sinned against You,”
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
My enemies say evil of me: When he dies—his name has perished!
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
And if he came to see—he speaks vanity, His heart gathers iniquity to itself, He goes out—at the street he speaks.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
All hating me whisper together against me, Against me they devise evil to me:
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
A worthless thing is poured out on him, And because he lay down he does not rise again.
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
Even my ally, in whom I trusted, One eating my bread, Made the heel great against me,
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
And You, YHWH, favor me, And cause me to rise, And I give repayment to them.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
By this I have known, That You have delighted in me, Because my enemy does not shout over me.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
As for me, in my integrity, You have taken hold on me, And cause me to stand before You for all time.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed [is] YHWH, God of Israel, From age to age. Amen and Amen.

< Zaburi 41 >