< Zaburi 41 >
1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
For the end, a Psalm of David. Blessed [is the man] who thinks, on the poor and needy: the Lord shall deliver him in an evil day.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
May the Lord preserve him and keep him alive, and bless him on the earth, and not deliver him into the hands of his enemy.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
May the Lord help him upon the bed of his pain; you have made all his bed in his sickness.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, O Lord, have mercy upon me; heal my soul; for I have sinned against you.
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
Mine enemies have spoken evil against me, [saying], When shall he die, and his name perish?
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
And if he came to see [me], his heart spoke vainly; he gathered iniquity to himself; he went forth and spoke in like manner.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
All my enemies whispered against me; against me they devised my hurt.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
They denounced a wicked word against me, [saying], Now that he lies, shall he not rise up again?
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
For even the man of my peace, in whom I trusted, who ate my bread, lifted up [his] heel against me.
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
But you, O Lord, have compassion upon me, and raise me up, and I shall requite them.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
By this I know that you have delighted in me, because mine enemy shall not rejoice over me.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
But you did help me because of [mine] innocence, and have established me before you for ever.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed [be] the Lord God of Israel from everlasting, and to everlasting. So be it, so be it.