< Zaburi 41 >
1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
Blessed is he that considers the poor: the LORD will deliver him in time of trouble.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
The LORD will preserve him, and keep him alive; and he shall be blessed on the earth: and you will not deliver him to the will of his enemies.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
The LORD will strengthen him on the bed of languishing: you will make all his bed in his sickness.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, LORD, be merciful to me: heal my soul; for I have sinned against you.
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
My enemies speak evil of me, When shall he die, and his name perish?
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
And if he come to see me, he speaks vanity: his heart gathers iniquity to itself; when he goes abroad, he tells it.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
All that hate me whisper together against me: against me do they devise my hurt.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
An evil disease, say they, sticks fast to him: and now that he lies he shall rise up no more.
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
Yes, my own familiar friend, in whom I trusted, which did eat of my bread, has lifted up his heel against me.
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
But you, O LORD, be merciful to me, and raise me up, that I may requite them.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
By this I know that you favor me, because my enemy does not triumph over me.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
And as for me, you uphold me in my integrity, and set me before your face for ever.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed be the LORD God of Israel from everlasting, and to everlasting. Amen, and Amen.