< Zaburi 41 >

1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
Unto the end, a psalm for David himself. Blessed is he that understandeth concerning the needy and the poor: the Lord will deliver him in the evil day.
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
The Lord preserve him and give him life, and make him blessed upon the earth: and deliver him not up to the will of his enemies.
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
The Lord help him on his bed of sorrow: thou hast turned all his couch in his sickness.
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said: O Lord, be thou merciful to me: heal my soul, for I have sinned against thee.
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
My enemies have spoken evils against me: when shall he die and his name perish?
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
And if he came in to see me, he spoke vain things: his heart gathered together iniquity to itself. He went out and spoke to the same purpose.
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
All my enemies whispered together against me: they devised evils to me.
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
They determined against me an unjust word: shall he that sleepeth rise again no more?
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
For even the man of peace, in whom I trusted, who ate my bread, hath greatly supplanted me.
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
But thou, O Lord, have mercy on me, and raise me up again: and I will requite them.
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
By this I know, that thou hast had a good will for me: because my enemy shall not rejoice over me.
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
But thou hast upheld me by reason of my innocence: and hast established me in thy sight for ever.
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
Blessed by the Lord the God of Israel from eternity to eternity. So be it. So be it.

< Zaburi 41 >