< Zaburi 41 >

1 Amebarikiwa mtu yule amkumbukaye mnyonge; katika siku ya taabu, Yahwe atamuokoa.
達味詩歌,交與樂官。 眷顧貧窮人的人,真是有福,患難時日,他必蒙上主救助。
2 Yahwe atamuhifadhi na kumuweka hai, naye atabarikiwa duniani; Yahwe hata mrudisha kwenye mapenzi ya adui zake.
上主必保護他,賜他生存,在世上蒙福,決不將他交給他的仇敵而任敵所欲。
3 Awapo kwenye kitanda cha mateso Yahwe atamsaidia; nawe utakifanya kitanda cha ugonjwa kuwa kitanda cha uponyaji.
他呻吟床榻,上主給他支援,他患病時,必使他轉危為安。
4 Nami nilisema, “Yahwe unihurumie! Uniponye, kwa maana nimekutenda dhambi wewe.”
我曾哀求你:上主,求你憐憫我」,求你治癒我,因為我得罪了你。
5 Adui zangu huongea maovu dhidi yangu, wakisema, 'Atakufa lini na jina lake lipotee?'
我的仇敵反而惡言辱罵我說:「他何時死,他的名字幾時泯滅?
6 Adui yangu ajapo kuniona, huongea mambo yasiyo na maana; moyo wake hukusanya maafa yangu kwa ajili yake mwenyewe; na aondokapo kwangu, yeye huwaambia watu wengine kuhusu hayo.
前來訪我的人,只以虛言相待,其實是心懷惡意,出去便說出來。
7 Wale wote wanaonichukia kwa pamoja hunon'gona dhidi yangu; nao wanafarijika kwa ajili ya maumivu yangu.
恨我的人,個個竊竊私議,咒我遭殃生疾:
8 Wakisema, “Gonjwa baya limemshikilia yeye haswa; na sasa kuwa amelala kitandani, hatainuka kamwe.”
願他身患惡疾! 願他一病不起!
9 Kweli, hata rafiki yangu wa karibu, ambae nilimuamini, aliye kula mkate wangu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.
連我素來信賴的知心友好,吃過我飯的人,也舉腳踢我。
10 Bali wewe, Yahwe, unihurumie na uniinue ili kwamba niwalipizie kisasi.
上主,求你可憐我,使我病除,為使我能對他們加以復仇。
11 Na hivi nitajua kuwa unafurahishwa nami, kwa kuwa adui yangu hatafurahia kunishinda.
我以此作為你真愛我的記號:就是不讓我的敵人向我誇耀;
12 Kwangu mimi, wewe unanisaidia katika uadilifu wangu na utaniweka mbele ya uso wako milele.
你時常保持我無災無難,使我永遠站在你的面前。
13 Yahwe, Mungu wa Israeli asifiwe milele na milele. Amen na Amen. Kitabu ya Pili
願上主,以色列天主,受讚頌,自永遠直到永遠,阿們,阿們

< Zaburi 41 >