< Zaburi 4 >

1 Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
For the leader, with stringed instruments. A psalm of David. Answer my cry, God, my defender. Often from straits you have brought me to spacious places. So now show me your favor and hear my prayer.
2 Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
How long, you proud people, will my honor be stained by the slanders you love, and the lies that you follow? (Selah)
3 Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
See! The Lord has shown me his wonderful kindness: the Lord hears, when I call to him.
4 Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
Sin not in your anger: but speak in your heart on your bed, and be still. (Selah)
5 Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
Offer true sacrifice, trust in the Lord.
6 Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
Many are longing for fortune to smile. Lift upon us the light of your face.
7 Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
You have put in my heart, Lord, a deeper joy than was theirs who had corn and wine in abundance.
8 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.
So in peace I will lie down and sleep; for you, Lord, keep me safe.

< Zaburi 4 >