< Zaburi 4 >

1 Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
To him that excelleth on Neginoth. A Psalme of Dauid. Heare me when I call, O God of my righteousnes: thou hast set me at libertie, when I was in distresse: haue mercie vpon me and hearken vnto my prayer.
2 Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
O ye sonnes of men, howe long will yee turne my glory into shame, louing vanitie, and seeking lyes? (Selah)
3 Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
For be ye sure that the Lord hath chosen to himselfe a godly man: the Lord will heare when I call vnto him.
4 Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
Tremble, and sinne not: examine your owne heart vpon your bed, and be still. (Selah)
5 Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
Offer the sacrifices of righteousnes, and trust in the Lord.
6 Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
Many say, Who will shewe vs any good? but Lord, lift vp the light of thy countenance vpon vs.
7 Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
Thou hast giuen mee more ioye of heart, then they haue had, when their wheate and their wine did abound.
8 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.
I will lay mee downe, and also sleepe in peace: for thou, Lord, onely makest me dwell in safetie.

< Zaburi 4 >