< Zaburi 38 >

1 Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
Salmo di Davide. Per far ricordare. O Eterno, non mi correggere nella tua ira, e non castigarmi nel tuo cruccio!
2 Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
Poiché le tue saette si sono confitte in me, e la tua mano m’è calata addosso.
3 Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
Non v’è nulla d’intatto nella mia carne a cagion della tua ira; non v’è requie per le mie ossa a cagion del mio peccato.
4 Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
Poiché le mie iniquità sorpassano il mio capo; son come un grave carico, troppo pesante per me.
5 Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
Le mie piaghe son fetide e purulenti per la mia follia.
6 Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
Io son tutto curvo e abbattuto, vo attorno tuttodì vestito a bruno.
7 Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
Poiché i miei fianchi son pieni d’infiammazione, e non v’è nulla d’intatto nella mia carne.
8 Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
Son tutto fiacco e rotto; io ruggisco per il fremito del mio cuore.
9 Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
Signore, ogni mio desiderio è nel tuo cospetto, e i miei sospiri non ti son nascosti.
10 Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
Il mio cuore palpita, la mia forza mi lascia, ed anche la luce de’ miei occhi m’è venuta meno.
11 Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
I miei amici, i miei compagni stan lontani dalla mia piaga, e i miei prossimi si fermano da lungi.
12 Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
Quelli che cercan la mia vita mi tendono reti, e quelli che procurano il mio male proferiscon cose maligne e tutto il giorno meditano frodi.
13 Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
Ma io, come un sordo, non odo: son come un muto che non apre la bocca.
14 Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
Son come un uomo che non ascolta, e nella cui bocca non è replica di sorta.
15 Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
Poiché, in te io spero, o Eterno; tu risponderai, o Signore, Iddio mio!
16 Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
Io ho detto: Non si rallegrino di me; e quando il mio piè vacilla, non s’innalzino superbi contro a me.
17 Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
Perché io sto per cadere, e il mio dolore è del continuo davanti a me.
18 Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
Io confesso la mia iniquità, e sono angosciato per il mio peccato.
19 Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
Ma quelli che senza motivo mi sono nemici sono forti, quelli che m’odiano a torto son moltiplicati.
20 Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
Anche quelli che mi rendon male per bene sono miei avversari, perché seguo il bene.
21 Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
O Eterno, non abbandonarmi; Dio mio, non allontanarti da me;
22 Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.
affrettati in mio aiuto, o Signore, mia salvezza!

< Zaburi 38 >