< Zaburi 38 >

1 Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
大卫的纪念诗。 耶和华啊,求你不要在怒中责备我, 不要在烈怒中惩罚我!
2 Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
因为,你的箭射入我身; 你的手压住我。
3 Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
因你的恼怒,我的肉无一完全; 因我的罪过,我的骨头也不安宁。
4 Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
我的罪孽高过我的头, 如同重担叫我担当不起。
5 Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
因我的愚昧, 我的伤发臭流脓。
6 Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
我疼痛,大大拳曲, 终日哀痛。
7 Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
我满腰是火; 我的肉无一完全。
8 Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
我被压伤,身体疲倦; 因心里不安,我就唉哼。
9 Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
主啊,我的心愿都在你面前; 我的叹息不向你隐瞒。
10 Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
我心跳动,我力衰微, 连我眼中的光也没有了。
11 Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
我的良朋密友因我的灾病都躲在旁边站着; 我的亲戚本家也远远地站立。
12 Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
那寻索我命的设下网罗; 那想要害我的口出恶言, 终日思想诡计。
13 Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
但我如聋子不听, 像哑巴不开口。
14 Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
我如不听见的人, 口中没有回话。
15 Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
耶和华啊,我仰望你! 主—我的 神啊,你必应允我!
16 Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
我曾说:恐怕他们向我夸耀; 我失脚的时候,他们向我夸大。
17 Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
我几乎跌倒; 我的痛苦常在我面前。
18 Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
我要承认我的罪孽; 我要因我的罪忧愁。
19 Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
但我的仇敌又活泼又强壮, 无理恨我的增多了。
20 Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
以恶报善的与我作对, 因我是追求良善。
21 Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
耶和华啊,求你不要撇弃我! 我的 神啊,求你不要远离我!
22 Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.
拯救我的主啊,求你快快帮助我!

< Zaburi 38 >