< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
in finem servo Domini David dixit iniustus ut delinquat in semet ipso non est timor Dei ante oculos eius
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
quoniam dolose egit in conspectu eius ut inveniatur iniquitas eius ad odium
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
verba oris eius iniquitas et dolus noluit intellegere ut bene ageret
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
iniquitatem meditatus est in cubili suo adstetit omni viae non bonae malitiam autem non odivit
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Domine in caelo misericordia tua et veritas tua usque ad nubes
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
iustitia tua sicut montes Dei iudicia tua abyssus multa homines et iumenta salvabis Domine
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
quemadmodum multiplicasti misericordiam tuam Deus filii autem hominum in tegmine alarum tuarum sperabunt
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
inebriabuntur ab ubertate domus tuae et torrente voluntatis tuae potabis eos
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
quoniam apud te fons vitae in lumine tuo videbimus lumen
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
praetende misericordiam tuam scientibus te et iustitiam tuam his qui recto sunt corde
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
non veniat mihi pes superbiae et manus peccatoris non moveat me
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
ibi ceciderunt qui operantur iniquitatem expulsi sunt nec potuerunt stare

< Zaburi 36 >