< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
Pour le chef musicien. Par David, le serviteur de Yahvé. Une révélation est dans mon cœur au sujet de la désobéissance des méchants: Il n'y a pas de crainte de Dieu devant ses yeux.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
Car il se flatte à ses propres yeux, trop pour détecter et haïr son péché.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Les paroles de sa bouche ne sont qu'iniquité et tromperie. Il a cessé d'être sage et de faire le bien.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
Il complote l'iniquité sur son lit. Il se place d'une manière qui n'est pas bonne. Il ne déteste pas le mal.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Ta bonté, Yahvé, est dans les cieux. Votre fidélité s'étend jusqu'aux cieux.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Ta justice est comme les montagnes de Dieu. Vos jugements sont comme une grande profondeur. Yahvé, tu préserves l'homme et l'animal.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
Que ta bonté est précieuse, Dieu! Les enfants des hommes se réfugient à l'ombre de tes ailes.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
Ils seront abondamment satisfaits de l'abondance de ta maison. Tu les feras boire au fleuve de tes plaisirs.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
Car chez toi est la source de la vie. Dans ta lumière, nous verrons la lumière.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
Oh, continuez votre bonté envers ceux qui vous connaissent, ta justice à ceux qui ont le cœur droit.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Que le pied de l'orgueil ne vienne pas contre moi. Ne laisse pas la main des méchants me chasser.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
C'est làque sont tombés les ouvriers de l'iniquité. Ils sont poussés vers le bas, et ne pourront pas se relever.

< Zaburi 36 >