< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
For the chief musician. A psalm of David the servant of Yahweh. An evil man speaks of his transgression from deep in his heart, there is no fear of God in his eyes.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
For he comforts himself, thinking that his sin will not be discovered and be hated.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
His words are sinful and deceitful; he does not want to be wise and do good.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
While he lies in bed, he plans ways to sin; he sets out on an evil way; he does not reject evil.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Your covenant faithfulness, Yahweh, reaches to the heavens; your loyalty reaches to the clouds.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Your righteousness is like the mountains of God; your judgments are like the great deep. Yahweh, you preserve both mankind and the animals.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
How precious is your covenant faithfulness, God! Humanity takes refuge under the shadow of your wings.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
They feast upon the abundance of your house; you let them drink from the river of your delights.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
For with you is the fountain of life; in your light we will see light.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
Extend your covenant faithfulness fully to those who know you, your defense to the upright of heart.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Do not let the foot of the arrogant man come near to me. Do not let the hand of the wicked drive me away.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
Over there the evildoers have fallen; they are knocked down and are not able to get up.

< Zaburi 36 >