< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
“For the leader of the music. A psalm of David, the servant of the Lord.” To speak of the ungodliness of the wicked is in my heart. He hath no fear of God before his eyes.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
For he flattereth himself in his own eyes, Till his iniquity is found out and hated.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit; He neglecteth to be wise and to do good.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
He deviseth mischief upon his bed; He persevereth in an evil way; He abhorreth not sin.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Thy goodness, O LORD! reacheth to the heavens, And thy faithfulness to the clouds;
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Thy righteousness is like the high mountains; Thy judgments are a great deep; Thou, O LORD! preservest man and beast!
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
How precious is thy loving-kindness, O God! Yea, the sons of men seek refuge under the shadow of thy wings.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
They are satisfied with the abundance of thy house, And thou causest them to drink of the full stream of thy pleasures.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
For with thee is the fountain of life; Through thy light we see light.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
O continue thy loving-kindness to them that know thee, And thy favor to the upright in heart!
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Let not the foot of the proud come upon me, Nor the hand of the wicked remove me!
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
Lo! already are the workers of iniquity fallen; They are cast down; they are unable to rise!

< Zaburi 36 >