< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
“To the chief musician, by the servant of the Lord, by David.” Saith vice itself to the wicked—so I feel it within my heart— that he should have no dread of God before his eyes.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
For he flattereth himself in his own eyes [too much] to find out his iniquity to hate it.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are wickedness and deceit: he hath left off to be wise, to do good.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
He deviseth wickedness upon his couch; he placeth himself on a way that is not good; evil he despiseth not.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
O Lord, into the heavens reacheth thy kindness, thy faithfulness even into the skies.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Thy righteousness is like the mountains of God; thy acts of justice like the great deep: man and beast dost thou ever help, O Lord.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
How precious is thy kindness, O God! And the children of men that seek shelter under the shadow of thy wings, —
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
These will be abundantly satisfied with the fatness of thy house; and of the stream of thy delights wilt thou give them to drink.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
For with thee is the source of life: in thy light shall we see light.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
Draw down continuously thy kindness unto those that acknowledge thee; and thy righteousness to the upright in heart.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Let not come against me the foot of pride, and let not the hand of the wicked chase me off.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
There are fallen the workers of wickedness: they are thrust down, and shall not be able to rise.

< Zaburi 36 >