< Zaburi 34 >

1 Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
Salmo de David, cuando mudó su semblante delante de Abimelech, y él lo echó, y fuése. BENDECIRÉ á Jehová en todo tiempo; su alabanza [será] siempre en mi boca.
2 Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
En Jehová se gloriará mi alma: oiránlo los mansos, y se alegrarán.
3 Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
Engrandeced á Jehová conmigo, y ensalcemos su nombre á una.
4 Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
Busqué á Jehová, y él me oyó, y libróme de todos mis temores.
5 Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
A él miraron y fueron alumbrados: y sus rostros no se avergonzaron.
6 Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
Este pobre clamó, y oyóle Jehová, y librólo de todas sus angustias.
7 Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
El ángel de Jehová acampa en derredor de los que le temen, y los defiende.
8 Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
Gustad, y ved que es bueno Jehová: dichoso el hombre que confiará en él.
9 Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
Temed á Jehová, vosotros sus santos; porque no hay falta para los que le temen.
10 Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
Los leoncillos necesitaron, y tuvieron hambre; pero los que buscan á Jehová, no tendrán falta de ningún bien.
11 Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
Venid, hijos, oidme; el temor de Jehová os enseñaré.
12 Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
¿Quién es el hombre que desea vida, que codicia días para ver bien?
13 Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
Guarda tu lengua de mal, y tus labios de hablar engaño.
14 Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
Apártate del mal, y haz el bien; busca la paz, y síguela.
15 Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
Los ojos de Jehová están sobre los justos, y [atentos] sus oídos al clamor de ellos.
16 Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
La ira de Jehová contra los que mal hacen, para cortar de la tierra la memoria de ellos.
17 Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
Clamaron [los justos], y Jehová oyó, y librólos de todas sus angustias.
18 Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
Cercano está Jehová á los quebrantados de corazón; y salvará á los contritos de espíritu.
19 Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
Muchos son los males del justo; mas de todos ellos lo librará Jehová.
20 Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
El guarda todos sus huesos; ni uno de ellos será quebrantado.
21 Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
Matará al malo la maldad; y los que aborrecen al justo serán asolados.
22 Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.
Jehová redime el alma de sus siervos; y no serán asolados cuantos en él confían.

< Zaburi 34 >