< Zaburi 34 >
1 Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
Pesem Davidova, ko je bil izpremenil lice svoje pred Abimelekom, in je bil odšel, ker ga je on podil. Blagoslavljal bodem Gospoda vsak čas; vedno bode hvala njegova v ustih mojih.
2 Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
V Gospodu se bode ponašala duša moja; čuli bodejo krotki ter se veselili;
3 Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
Poveličujte Gospoda z menoj, in vkup povišujmo ime njegovo.
4 Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
Iskal sem Gospoda in uslišal me je, in iz vseh strahov mojih me je rešil.
5 Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
Kateri gledajo vanj in pritekajo, obličja njih naj se ne osramoté, govoré naj:
6 Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
Ta ubogi je klical, in Gospod je uslišal; in rešil ga je iz vseh stisek njegovih.
7 Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
Šatorišče stavijo angeli Gospodovi okrog njih, kateri se ga bojé, in otme jih.
8 Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
Pokusite in vidite, da je dober Gospod; blagor možu, kateri pribega k njemu.
9 Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
Bojte se Gospoda, svetniki njegovi, ker stradanja ni njim, ki se ga bojé.
10 Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
Mladi levi beračijo in stradajo; kateri pa iščejo Gospoda, ne pogrešajo nobenega blaga.
11 Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
Dejte, sinovi, poslušajte me: strah Gospodov vas bodem učil.
12 Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
Kdo je ón mož, kateri se veseli življenja, ljubi dní, rad uživa dobro?
13 Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
Varuj jezik svoj hudega, in ustne tvoje naj ne govoré zvijače.
14 Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
Umikaj se hudemu in delaj dobro; išči mirú in hodi za njim.
15 Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
Oči Gospodove pazijo na pravične, in ušesa njegova na njih vpitje.
16 Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
Srdito pa je njim, ki delajo hudo, obličje Gospodovo, da iztrebi sè zemlje njihov spomin.
17 Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
Ko kličejo, sliši jih Gospod, in jih iz vseh njih stisek otima.
18 Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
Blizu je Gospod pobitim v srci; in potrte v duhu rešuje.
19 Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
Mnoge so pravičnega nadloge, ali iz njih vseh ga reši Gospod:
20 Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
Vse kosti njegovo ohrani, ena izmed njih se ne zlomi.
21 Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
Krivične pa zadeva sè smrtjo nadloga, in kateri sovražijo pravičnega, pogubé se.
22 Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.
Gospod otima dušo hlapcev svojih, in ne pogubi se nobeden, ki pribega k njemu.