< Zaburi 34 >

1 Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
I will bless Jehovah at all times. His praise shall continually be in my mouth.
2 Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
My soul shall make its boast in Jehovah. The humble shall hear of it, and be glad.
3 Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
O magnify Jehovah with me, and let us exalt his name together.
4 Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
I sought Jehovah, and he answered me, and delivered me from all my fears.
5 Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
They looked to him, and were radiant, and their faces shall never be confounded.
6 Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
This poor man cried, and Jehovah heard him, and saved him out of all his troubles.
7 Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
The agent of Jehovah encamps round about those who fear him, and delivers them.
8 Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
O taste and see that Jehovah is good. Blessed is the man who takes refuge in him.
9 Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
O fear Jehovah, ye his sanctified, for there is no want to those who fear him.
10 Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
The young lions do lack, and suffer hunger, but those who seek Jehovah shall not want any good thing.
11 Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
Come, ye children, hearken to me. I will teach you the fear of Jehovah.
12 Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
What man is he who desires life, and loves many days, that he may see good?
13 Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
Keep thy tongue from evil, and thy lips from speaking deceit.
14 Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
Depart from evil, and do good. Seek peace, and pursue it.
15 Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
The eyes of Jehovah are toward the righteous, and his ears are open to their prayer.
16 Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
(The face of Jehovah is against those who do evil, to cut off the remembrance of them from the earth.)
17 Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
They cried, and Jehovah heard, and delivered them out of all their troubles.
18 Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
Jehovah is near to those who are of a broken heart, and saves such as are of a contrite spirit.
19 Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
Many are the afflictions of the righteous, but Jehovah delivers him out of them all.
20 Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
He keeps all his bones. Not one of them is broken.
21 Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
Evil shall kill the wicked, and those who hate the righteous shall be condemned.
22 Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.
Jehovah redeems the soul of his servants, and none of those who take refuge in him shall be condemned.

< Zaburi 34 >