< Zaburi 32 >
1 Zaburi ya Daudi. Zaburi. Amebarikiwa mtu yule aliyesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimesitiriwa.
Благо ономе, коме је опроштена кривица, коме је грех покривен.
2 Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe hamuhesabii hatia na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Благо човеку, коме Господ не прима грехе и у чијем духу нема лукавства.
3 Nilipokaa kimya, mifupa yangu ilidhohofika huku nikiugua muda wote.
Кад ћутах, посахнуше кости моје од уздисања мог по вас дан.
4 Mchana na usiku mkono wako ulinielemea. nguvu zangu zilikauka wakati wa kiangazi. (Selah)
Јер дан и ноћ тишташе ме рука Твоја; неста сока у мени као на летњој припеци.
5 Ndipo nilipotambua makosa yangu kwako, nami sifichi tena uovu wangu. Nilisema, “Nitakiri makosa yangu kwa Yahwe,” nawe ulinisamehe hatia ya dhambi zangu. (Selah)
Грех свој казах Теби, и кривице своје не затајих; рекох: Исповедам Господу преступе своје; и Ти скиде с мене кривицу греха мог.
6 Kwa sababu ya haya, wale wote ambao ni wa kimungu wanapaswa kukuomba wakati wa shida kubwa. Nayo mafuriko yajapo, hayatawapata watu hao.
Зато нека Ти се моли сваки светац, кад се можеш наћи; и онда потоп велике воде неће га стигнути.
7 Wewe u mahali pangu pa kujifichia, nawe utanilinda matatizoni. Wewe utanizunguka pamoja na nyimbo zaushindi. (Selah)
Ти си заклон мој, Ти ме чуваш од тескобе; окружаваш ме радостима у избављању.
8 Nitakuelekeza na kukufundisha katika njia upasayo kuiendea. Nitakuelekeza huku macho yangu yakikutazama.
Уразумићу те, и показаћу ти пут којим да идеш; саветоваћу те, око је моје на теби.
9 Msiwe kama farasi au kama nyumbu, ambao hawana uelewa; ni kwa hatamu na lijamu tu unaweza kuwapeleka popote utakapo wao waende.
Немојте бити као коњ, као мазга без разума, којима уздом и жвалама ваља обуздати губицу, кад не иду к Теби.
10 Waovu wanahuzuni nyingi, bali uaminifu wa agano la Yahwe utamzunguka yule anaye mwamini yeye.
Много муке има безбожник, а који се узда у Господа, око Њега је милост.
11 Furahini katika Yahwe, na mshangilie, ninyi wenye haki; pigeni kelele za shangwe, ninyi nyote wenye haki mioyoni mwenu.
Радујте се о Господу, и певајте, праведници; веселите се сви који сте правог срца.