< Zaburi 31 >
1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
Til sangmesteren; en salme av David. Til dig, Herre, tar jeg min tilflukt. La mig aldri i evighet bli til skamme, frels mig ved din rettferdighet!
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Bøi ditt øre til mig, skynd dig og redd mig, vær mig et klippevern, en borg til å frelse mig!
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
For du er min klippe og min borg, og for ditt navns skyld vil du føre og lede mig.
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
Du vil føre mig ut av garnet som de lønnlig har lagt for mig; for du er mitt vern.
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
I din hånd overgir jeg min ånd; du forløser mig, Herre, du trofaste Gud.
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
Jeg hater dem som akter på tomme avguder, men jeg, jeg setter min lit til Herren.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
Jeg vil fryde og glede mig over din miskunnhet, at du har sett min elendighet, aktet på min sjels trengsler;
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
du har ikke overgitt mig i fiendehånd, du har satt mine føtter på et rummelig sted.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Vær mig nådig, Herre! for jeg er i trengsel; borttæret av sorg er mitt øie, min sjel og mitt legeme.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
For mitt liv svinner bort med sorg, og mine år med sukk; min kraft er brutt for min misgjernings skyld, og mine ben er uttæret.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
For alle mine fienders skyld er jeg blitt til stor spott for mine naboer og til en skrekk for mine kjenninger; de som ser mig på gaten, flyr for mig.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
Jeg er glemt og ute av hjertet som en død, jeg er blitt som et ødelagt kar.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
For jeg hører baktalelse av mange, redsel fra alle kanter, idet de rådslår sammen imot mig; de lurer på å ta mitt liv.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
Men jeg, jeg setter min lit til dig, Herre! Jeg sier: Du er min Gud.
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
I din hånd er mine tider; redd mig av mine fienders hånd og fra mine forfølgere!
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
La ditt åsyn lyse over din tjener, frels mig ved din miskunnhet!
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol )
Herre, la mig ikke bli til skamme! for jeg kaller på dig. La de ugudelige bli til skamme, bli tause i dødsriket! (Sheol )
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
La løgnens leber bli målløse, som taler frekt imot den rettferdige med overmot og forakt!
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
Hvor stor din godhet er, som du har gjemt for dem som frykter dig, som du har vist mot dem som tar sin tilflukt til dig, for menneskenes barns øine!
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
Du skjuler dem i ditt åsyns skjul for menneskers sammensvergelser, du gjemmer dem i en hytte for tungers kiv.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Lovet være Herren! for han har underlig vist sin miskunnhet imot mig i en fast by.
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
Og jeg, jeg sa i min angst: Jeg er revet bort fra dine øine. Dog hørte du mine inderlige bønners røst, da jeg ropte til dig.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
Elsk Herren, alle I hans fromme! Herren vokter de trofaste og gjengjelder rikelig den som farer overmodig frem.
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Vær ved godt mot, og eders hjerte være sterkt, alle I som venter på Herren!