< Zaburi 31 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
For the chief musician. A psalm of David. In you, Yahweh, I take refuge; never let me be humiliated. Rescue me in your righteousness.
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Listen to me; rescue me quickly; be my rock of refuge, a stronghold to save me.
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
For you are my rock and my fortress; therefore for your name's sake, lead and guide me.
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
Pluck me out of the net that they have hidden for me, for you are my refuge.
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
Into your hands I entrust my spirit; you will redeem me, Yahweh, God of trustworthiness.
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
I hate those who serve worthless idols, but I trust in Yahweh.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
I will be glad and rejoice in your covenant faithfulness, for you saw my affliction; you knew the distress of my soul.
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
You have not given me into the hand of my enemy. You have set my feet in a wide open place.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Have mercy upon me, Yahweh, for I am in distress; my eyes grow weary with grief with my soul and my body.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
For my life is weary with sorrow and my years with groaning. My strength fails because of my sin, and my bones are wasting away.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
Because of all my enemies, people disdain me; my neighbors are appalled at my situation, and those who know me are horrified. Those who see me in the street run from me.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
I am forgotten as a dead man whom no one thinks about. I am like a broken pot.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
For I have heard the whispering of many, terrifying news from every side as they plot together against me. They plot to take away my life.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
But I trust in you, Yahweh; I say, “You are my God.”
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
My times are in your hand. Rescue me from the hands of my enemies and from those who pursue me.
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
Make your face shine on your servant; save me in your covenant faithfulness.
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
Do not let me be humiliated, Yahweh; for I call out to you! May the wicked be humiliated! May they be silent in Sheol. (Sheol h7585)
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
May lying lips be silenced that speak against the righteous defiantly with arrogance and contempt.
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
How great is your goodness that you have stored up for those who revere you, that you perform for those who take refuge in you before all the children of mankind!
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
In the shelter of your presence, you hide them from the plots of men. You hide them in a shelter from the violence of tongues.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Blessed be Yahweh, for he showed me his marvelous covenant faithfulness when I was in a besieged city.
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
Though I said in my haste, “I am cut off from your eyes,” yet you heard my plea for help when I cried to you.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
Oh, love Yahweh, all you faithful followers. Yahweh protects the faithful, but he pays back the arrogant in full.
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Be strong and confident, all you who trust in Yahweh for help.

< Zaburi 31 >