< Zaburi 31 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
“For the leader of the music. A psalm of David.” In thee, O LORD! do I trust; let me never be put to shame; According to thy goodness deliver me!
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Bow down thine ear to me; help me speedily! Be to me a strong rock, a high fortress, for my deliverance!
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
For thou art my rock and my high fortress; Be thou also my guide, and lead me, for thy name's sake!
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
Draw me out of the net which they have secretly laid for me, For thou art my strength!
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
Into thy hand I commit my life; Thou wilt deliver me, O LORD, thou God of truth!
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
I hate those who regard lying vanities, And put my trust in the LORD.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
I will be glad and rejoice in thy mercy, That thou hast looked upon my trouble, And hast had regard to my distress;
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
That thou hast not given me up to the hands of my enemies, But hast set my feet in a wide place.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Have mercy upon me, O LORD! for I am in trouble! My face is consumed with grief; Yea, my spirit and my body.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
For my life is wasted with sorrow, And my years with sighing; My strength faileth by reason of my affliction, And my bones are consumed on account of all my enemies.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
I have become the scorn of my neighbors, And the terror of my acquaintance; They who see me abroad flee from me.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
I am forgotten like a dead man out of mind; I am like a broken vessel.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
I hear the slander of many; fear is on every side; For they take counsel together against me; They devise to take away my life.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
But I trust in thee, O Jehovah! I say, “Thou art my God!”
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
My destiny is in thy hand; Deliver me from the power of my enemies and persecutors!
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
Let thy face shine upon thy servant, And save me through thy mercy!
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
Let me not be put to shame, O LORD! for I have called upon thee; Let the wicked be put to shame; Let them be silenced in the grave! (Sheol h7585)
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
Let lying lips be put to silence, Which speak proud things against the righteous, With haughtiness and contempt!
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
O how great is thy goodness, which thou treasurest up for them that fear thee; Which thou showest to them that trust in thee, before the sons of men!
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
Thou hidest them in the secret place of thy presence from the machinations of men; Thou shelterest them in thy pavilion from the violence of tongues.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Praised be the LORD; for he hath shown me his wonderful kindness, As in a fortified city!
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
I said in my distress, “I am cut off from before thine eyes;” But thou didst hear the voice of my supplication, When I cried unto thee.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
O love the LORD, all ye his servants; For the LORD preserveth the faithful, And requiteth the proud in full measure!
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Be of good courage; let your hearts be strong, All ye who trust in the LORD!

< Zaburi 31 >