< Zaburi 3 >
1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
Un salmo de David, cuando huyó de su hijo Absalón. ¡Yahvé, cómo han aumentado mis adversarios! Muchos son los que se levantan contra mí.
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Son muchos los que dicen de mi alma, “No hay ayuda para él en Dios”. (Selah)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
Pero tú, Yahvé, eres un escudo a mi alrededor, mi gloria, y el que levanta mi cabeza.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
Clamo a Yahvé con mi voz, y me responde desde su santo monte. (Selah)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
Me acosté y dormí. Me he despertado, porque Yahvé me sostiene.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
No tendré miedo de decenas de miles de personas que se han puesto en mi contra por todos lados.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
¡Levántate, Yahvé! ¡Sálvame, Dios mío! Porque has golpeado a todos mis enemigos en el pómulo. Has roto los dientes de los malvados.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
La salvación pertenece a Yahvé. Que tu bendición sea para tu pueblo. (Selah)