< Zaburi 3 >

1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
[Ein Psalm von David, als er vor seinem Sohne Absalom floh.] Jehova! wie viele sind meiner Bedränger! Viele erheben sich wider mich;
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Viele sagen von meiner Seele: Es ist keine Rettung für ihn bei [W. in] Gott! (Sela) [Bedeutet wahrsch.: (Zwischenspiel) od. Verstärkung der begleitenden Musik]
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
Du aber, Jehova, bist ein Schild um mich her, meine Herrlichkeit, [O. Ehre] und der mein Haupt emporhebt.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
Mit meiner Stimme rufe ich zu Jehova, und er antwortet mir von seinem heiligen Berge. (Sela)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
Ich legte mich nieder und schlief; ich erwachte, denn Jehova stützt mich.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
Nicht fürchte ich mich vor Zehntausenden des Volkes, die sich ringsum wider mich gesetzt haben.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Stehe auf, Jehova! rette mich, mein Gott! denn du hast alle meine Feinde auf den Backen geschlagen; die Zähne der Gesetzlosen hast du zerschmettert.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Von Jehova ist die Rettung; dein Segen ist auf deinem Volke. [O. komme auf dein Volk] (Sela)

< Zaburi 3 >