< Zaburi 3 >

1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
Adonai, how my adversaries have increased! Many are those who rise up against me.
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Many there are who say of my soul, “There is no yishu'ah ·salvation· for him in God.” (Selah) ·contemplation with musical interlude·
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But you, Adonai, are a shield around me, my kavod ·weighty glory·, and the one who lifts up my head.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
I cry to Adonai with my voice, and he answers me out of his holy hill. (Selah) ·contemplation with musical interlude·
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I laid myself down and slept. I awakened; for Adonai sustains me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I will not be afraid of tens of thousands of people who have set themselves against me on every side.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Arise, Adonai! Save me, my God! For you have struck all of my enemies on the cheek bone. You have broken the teeth of the wicked.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Yishu'ah ·Salvation· belongs to Adonai. Your blessing be on your people. (Selah) ·contemplation with musical interlude·

< Zaburi 3 >