< Zaburi 3 >

1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
“A Psalm of David, when he fled from his son Absalom.” How many, O LORD, are mine enemies! How many are they who rise up against me!
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
How many are they who say of me, “There is no help for him with God”! (Pause)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But thou, O LORD! art my shield, My glory, and the lifter-up of my head.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
I call upon the LORD with my voice, And he heareth me from his holy hill. (Pause)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I lay me down and sleep; I awake, for the LORD sustaineth me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I will not fear the ten thousands of people Who on every side set themselves against me.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Arise, O LORD! Save me, O my God! For thou smitest the cheek of all my enemies; Thou breakest the teeth of the wicked.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Deliverance cometh from the LORD: May thy blessing be with thy people! (Pause)

< Zaburi 3 >