< Zaburi 3 >
1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
A Psalm of David, when he fled from Absalom his son. LORD, how many are mine adversaries become! Many are they that rise up against me.
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Many there are that say of my soul: 'There is no salvation for him in God.' (Selah)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But thou, O LORD, art a shield about me; my glory, and the lifter up of my head.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
With my voice I call unto the LORD, and He answereth me out of His holy mountain. (Selah)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I lay me down, and I sleep; I awake, for the LORD sustaineth me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I am not afraid of ten thousands of people, that have set themselves against me round about.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Arise, O LORD; save me, O my God; for Thou hast smitten all mine enemies upon the cheek, Thou hast broken the teeth of the wicked.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Salvation belongeth unto the LORD; Thy blessing be upon Thy people. (Selah)