< Zaburi 3 >
1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
A Psalme of Dauid, when he fled from his sonne Absalom. Lord, howe are mine aduersaries increased? howe many rise against me?
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Many say to my soule, There is no helpe for him in God. (Selah)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But thou Lord art a buckler for me: my glory, and the lifter vp of mine head.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
I did call vnto the Lord with my voyce, and he heard me out of his holy mountaine. (Selah)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I layed me downe and slept, and rose vp againe: for the Lord susteined me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I will not be afrayde for ten thousand of the people, that should beset me round about.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
O Lord, arise: helpe me, my God: for thou hast smitten all mine enemies vpon the cheeke bone: thou hast broken the teeth of the wicked.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Saluation belongeth vnto the Lord, and thy blessing is vpon thy people. (Selah)