< Zaburi 3 >

1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
A psalm of David concerning the time he had to flee from his son Absalom. Lord, my enemies have become so many; so many are rebelling against me.
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
So many are telling me, “God can't save you!” (Selah)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But you, Lord, are a shield protecting me. You give me victory; you hold my head high.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
I cry out to the Lord for help, and he answers me from his holy mountain. (Selah)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I lie down to sleep, and in the morning I wake up because the Lord takes care of me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I'm not afraid of tens of thousands who surround me, people who are against me.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Stand up for me, Lord! Save me, my God! Hit all my enemies on the cheek; break the teeth of the wicked!
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Salvation belongs to you, Lord; may you be a blessing to your people. (Selah)

< Zaburi 3 >