< Zaburi 3 >

1 Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
A Psalm of David, when he fled from the presence of his son Abessalom. O Lord, why are they that afflict me multiplied? many rise up against me.
2 Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
Many say concerning my soul, There is no deliverance for him in his God. (Pause)
3 Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
But thou, O Lord, art my helper: my glory, and the one that lifts up my head.
4 Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
I cried to the Lord with my voice, and he heard me out of his holy mountain. (Pause)
5 Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
I lay down and slept; I awaked; for the Lord will help me.
6 Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
I will not be afraid of ten thousands of people, who beset me round about.
7 Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
Arise, Lord; deliver me, my God: for thou hast smitten all who were without cause mine enemies; thou hast broken the teeth of sinners.
8 Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.
Deliverance is the Lord's, and thy blessing is upon thy people.

< Zaburi 3 >