< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Psalmus David, In consummatione tabernaculi. Afferte Domino filii Dei: afferte Domino filios arietum:
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Afferte Domino gloriam et honorem, afferte Domino gloriam nomini eius: adorate Dominum in atrio sancto eius.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
Vox Domini super aquas, Deus maiestatis intonuit: Dominus super aquas multas.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
Vox Domini in virtute: vox Domini in magnificentia.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
Vox Domini confringentis cedros: et confringet Dominus cedros Libani:
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
Et comminuet eas tamquam vitulum Libani: et dilectus quemadmodum filius unicornium.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
Vox Domini intercidentis flammam ignis:
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
vox Domini concutientis desertum: et commovebit Dominus desertum Cades.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
Vox Domini præparantis cervos, et revelabit condensa: et in templo eius omnes dicent gloriam.
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Dominus diluvium inhabitare facit: et sedebit Dominus rex in æternum.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
Dominus virtutem populo suo dabit: Dominus benedicet populo suo in pace.

< Zaburi 29 >