< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Psaume de David. Fils des Princes rendez à l'Eternel, rendez à l'Eternel la gloire et la force.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Rendez à l'Eternel la gloire due à son Nom; prosternez-vous devant l'Eternel dans son Sanctuaire magnifique.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
La voix de l'Eternel est sur les eaux, le [Dieu] Fort de gloire fait tonner; l'Eternel est sur les grandes eaux.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
La voix de l'Eternel est forte, la voix de l'Eternel est magnifique.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
La voix de l'Eternel brise les cèdres, même l'Eternel brise les cèdres du Liban,
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
Et les fait sauter comme un veau: [il fait sauter] le Liban et Sirion, comme un faon de licorne.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
La voix de l'Eternel jette des éclats de flamme de feu.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
La voix de l'Eternel fait trembler le désert, l'Eternel fait trembler le désert de Kadès.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
La voix de l'Eternel fait faonner les biches, et découvre les forêts; mais quant à son Palais, chacun l'y glorifie.
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
L'Eternel a présidé sur le déluge; et l'Eternel présidera comme Roi éternellement.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
L'Eternel donnera de la force à son peuple; l'Eternel bénira son peuple en paix.

< Zaburi 29 >