< Zaburi 29 >
1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
melody to/for David to give to/for LORD son: type of god to give to/for LORD glory and strength
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
to give to/for LORD glory name his to bow to/for LORD in/on/with adornment holiness
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
voice LORD upon [the] water God [the] glory to thunder LORD upon water many
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
voice LORD in/on/with strength voice LORD in/on/with glory
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
voice LORD to break cedar and to break LORD [obj] cedar [the] Lebanon
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
and to skip about them like calf Lebanon and Sirion like son: young animal wild ox
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
voice LORD to hew flame fire
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
voice LORD to twist: tremble wilderness to twist: tremble LORD wilderness Kadesh
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
voice LORD to twist: dance doe and to strip wood and in/on/with temple his all his to say glory
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
LORD to/for flood to dwell and to dwell LORD king to/for forever: enduring
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
LORD strength to/for people his to give: give LORD to bless [obj] people his in/on/with peace