< Zaburi 29 >
1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
A Psalm of David. Give unto the LORD, O ye sons of the mighty, give unto the LORD glory and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Give unto the LORD the glory due unto his name; worship the LORD in the beauty of holiness.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The voice of the LORD is upon the waters: the God of glory thundereth, even the LORD upon many waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The voice of the LORD is powerful; the voice of the LORD is full of majesty.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The voice of the LORD breaketh the cedars; yea, the LORD breaketh in pieces the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
He maketh them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young wild-ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The voice of the LORD cleaveth the flames of fire.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The voice of the LORD shaketh the wilderness; the LORD shaketh the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The voice of the LORD maketh the hinds to calve, and strippeth the forests bare: and in his temple every thing saith, Glory.
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
The LORD sat [as king] at the Flood; yea, the LORD sitteth as king for ever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
The LORD will give strength unto his people; the LORD will bless his people with peace.