< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
A psalm of David. Ascribe to the Lord, you heavenly beings, ascribe to the Lord glory and power
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Ascribe to the Lord the glory he manifests: bow to the Lord in holy array.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The Lord’s voice peals on the waters. The God of glory has thundered. He peals o’er the mighty waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The Lord’s voice sounds with strength, the Lord’s voice sounds with majesty.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The Lord’s voice breaks the cedars, he breaks the cedars of Lebanon,
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
making Lebanon dance like a calf, Sirion like a young wild ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The Lord’s voice hews out flames of fire.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The Lord’s voice rends the desert, he rends the desert of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The Lord’s voice whirls the oaks, and strips the forests bare; and all in his temple say “Glory.”
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
The Lord was king at the flood, the Lord sits throned forever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
The Lord gives strength to his people, he blesses his people with peace.

< Zaburi 29 >