< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
“A psalm of David.” Give to Jehovah, O ye sons of God! Give to Jehovah glory and praise!
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Give to Jehovah the glory due to his name; Worship Jehovah in holy attire!
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The voice of Jehovah is heard above the waters; The God of glory thundereth, -Jehovah above the great waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The voice of Jehovah is powerful; The voice of Jehovah is full of majesty;
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The voice of Jehovah breaketh the cedars; Yea, Jehovah breaketh the cedars of Lebanon;
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
Yea, he maketh them to leap like a calf, —Lebanon and Sirion like a young buffalo.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The voice of Jehovah divideth the flames of fire.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The voice of Jehovah maketh the wilderness tremble; Yea, Jehovah maketh the wilderness of Kadesh tremble.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The voice of Jehovah maketh the hinds bring forth, And layeth bare the forests; While, in his palace, every one declareth his glory.
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Jehovah sitteth above the flood; Yea, Jehovah sitteth king for ever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
Jehovah will give strength to his people; Jehovah will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >