< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
[A Psalm by David.] Ascribe to the LORD, you sons of the mighty, ascribe to the LORD glory and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Ascribe to the LORD the glory due to his name. Worship the LORD in holy array.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The voice of the LORD is on the waters. The God of glory thunders, even the LORD on many waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The voice of the LORD is powerful. The voice of the LORD is full of majesty.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The voice of the LORD breaks the cedars. Yes, the LORD breaks in pieces the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The voice of the LORD strikes with flashes of lightning.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The voice of the LORD shakes the wilderness. The LORD shakes the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The voice of the LORD makes the large trees tremble, and strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory."
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
The LORD sat enthroned at the Flood. Yes, the LORD sits as King forever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
The LORD will give strength to his people. The LORD will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >