< Zaburi 29 >
1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
[A Psalm by David.] Ascribe to Jehovah, you sons of the mighty, ascribe to Jehovah glory and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Ascribe to Jehovah the glory due to his name. Worship Jehovah in holy array.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The voice of Jehovah is on the waters. The God of glory thunders, even Jehovah on many waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The voice of Jehovah is powerful. The voice of Jehovah is full of majesty.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The voice of Jehovah breaks the cedars. Yes, Jehovah breaks in pieces the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The voice of Jehovah strikes with flashes of lightning.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The voice of Jehovah shakes the wilderness. Jehovah shakes the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The voice of Jehovah makes the large trees tremble, and strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory."
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Jehovah sat enthroned at the Flood. Yes, Jehovah sits as King forever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
Jehovah will give strength to his people. Jehovah will bless his people with peace.