< Zaburi 29 >
1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
A psalm of David. Honor the Lord, children of God, honor his glory and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Honor the Lord for his glorious character, bow in reverence to the Lord in his brilliant holiness.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The Lord's voice sounds over the sea. The God of glory thunders. The Lord thunders over the vast ocean.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The Lord's voice is powerful; the Lord's voice is majestic;
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
the Lord's voice shatters the cedars, even breaking the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
He makes the mountains of Lebanon skip like a calf, and Mount Hermon like a young wild ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The Lord's voice blazes out like lightning flashes.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The Lord's voice causes an earthquake in the desert; the desert of Kadesh shakes.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The Lord's voice makes the pregnant deer go into labor; it strips bare the forests. In his Temple all the worshipers shout, “Glory!”
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
The Lord sits on his throne above the floodwaters; the Lord is the eternal King.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
The Lord gives strength to his people; the Lord blesses them with peace.